Licha ya kuwepo kwa
  malalamiko mengi kutoka kwa
  wasanii wa filamu Bongo kuwa
  wanapata maslahi kiduchu
  kutoka katika kazi hiyo nguli wa
  maingizo kupitia vichekesho King
  Majuto ameanika hadharani
  lundo ma mali alizovuna
  kutokana na fani hiyo.
  Aliojiwa na teentz.com juzi
  kati Mzee Majuto alitanabaisha
  kuwa licha ya kuwepo kwa
  dhuluma nyingi kutoka kwa watu
  wanajiita wadaau wa filamu
  lakini amefanikiwa kuvuna
  nyumba na magari kadhaa
  kutoka katika kazi yake hiyo
  aliyoifanya kwa miaka zaidi ya 35
  sasa.
  "Ni kweli haki zetu nyingi
  zinapotea, lakini nashukuru
  mungu kwa miaka zaidi ya 35
  niliyofanya kazi ya uigizaji
  nimefanikiwa kujenga nyumba
  moja kubwa ambayo pia ina
  sehemu kubwa ya wazi huku pia
  nikifanikiwa kununua magari
  mawili moja likiwa la kisasa pia
  namiliki biashara kadhaa binafsi
  na hivi karibuni nimefungua
  kampuni yangu ya kurekodi
  filamu" alisema Majuto
  Story kutoka www.teentz.com
Tuesday, October 30, 2012
HUU NDO UTAJIRI WA KING MAJUTO BAADA YA KUKAA KWENYE GAME ZAID YA MIAKA 35
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment