Habari kutoka Kariakoo ameripoti kwamba makundi ya wananchi ambao wapo Kariakoo
 yameanza kuondoka Kariakoo kuelekea majumbani kwa sababu hali sio 
nzuri, polisi wametanda kwenye barabara zote ambapo magari yanayotoka 
sehemu mbalimbali kuingia mjini yamezuiwa kuingia kutokana na kikundi 
cha waandamanaji kilichojiandaa kuandamana kuelekea kwenye ofisi ya 
Waziri mkuu kutawanyishwa kwa mabomu ya machozi na kikundi 
kikasambaratika.
Polisi bado wanaendelea 
kudumisha ulinzi ambapo kwa sasa  maduka yamefungwa na mengine 
yanaendelea kufungwa, shughuli nyingine za kawaida zimesimama na kwa 
sasa msururu wa watu unarudi kuelekea majumbani, vikundi vya maandamano 
vimeripotiwa kujikusanya kwenye maeneo tofauti tofauti.
Polisi wanatumia Farasi, Mbwa 
na magari kusimamia amani ambapo vikundi vilivyojaribu kuandamana 
vilikua na bendera na wengine walikua na fimbo kabisa, na walikua na 
gari maalum ambalo walikua wamepanga ndio walitumie kwenda mjini kwenye 
ofisi ya waziri mkuu lakini polisi wakawawahi na kuwasambaratisha.

No comments:
Post a Comment